
SHANGA TISA EP: 20 MTUNZI: ASHROUPH K.A {TAYLOR PERRY WA TZ} MARA baada ya onyesho hilo la siri kutamatika na wateja kutawanyika. Kuna wateja wawili walimjilia Kadra na kumtaka huduma nyingine spesho! Wateja hao walikuwa, ni mzungu mmoja na mwarabu mmoja. "Jina yako sikia waitwa Kadra, au iko kosea mimi!?". Yule mzungu aliongea kwa kiswahili chake kibovu kibovu, ingawa ujumbe ulifika. "Ndio, Kadra ndo jina langu miye!". "Ok, taka wewe siku nzima iliyobakia toka sasa. Tukapumzike jumbani kwangu. Talipa wewe a lot of money!". Kadra alitabasam, kisha akatupia jicho upande wa pili, akamuona Chausiku akiwa anampiga chabo. Chausiku akamtikisia kichwa
No comments:
Post a Comment