
SHANGA TISA EP: {02} MTUNZI: ASHROUPH K.A {TAYLOR PERRY WA TZ} WALA haikuwachukua kitambo kirefu sana kufika nyumbani hapo kwa Bwena. Kwani hapa kuwa mbali kivile, tena ukizingatia walitumia usafiri wa haraka wa bodaboda. Pengo alifunga brek nje kabisa ya geti la nyumba ya Bwena. Kisha akaminya kengele maalumu, geti likafunguliwa, na aliyefungua si mwingine bali ni Bwena. "Ohoo. Karibuni ndani, karibuni sana. Pengo huyu ndo yule mgeni wangu?". "Ndio boss, huyu ndo Bahati buana! Mtoto mdogo mwenye nyota zake nzito mjini hapa. We mtizame tu kwa wasiwasi, kisa kajitanda hizo nikabu na baibui, ila akijitandua? Sijui..moto utawaka!'. Pengo alijitahidi
No comments:
Post a Comment