
PENZI LA MHALIFU 23. Siku kadhaa zilipita, nakumbuka ilikuwa ni siku ya jumamosi na ilikuwa ni mida ya saa moja jioni, siku hiyo nilikuwa nikitembea peke yangu huku nikiwa nimevaa nguo za kawaida tu na kwakuwa nilikuwa bado sijayazoea vizuri mazingira nilifika kwenye uchochoro na kukutana na kundi la vijana waliokuwa wakivuta bangi. Japo nilikuwa asikari ila niliogopa baada ya kuwaona vijana waliokuwa wakivuta bangi na ukizangatia nilikuwa kwenye mazingira hatarishi kidogo. Sikutaka kuwasemesha zaidi ya kuendelea na safari yangu ila kijana mmoja aliniita na mimi nilijifanya kama sijamsikia. Kijana aliyekuwa akiniita alikasirika baada ya kuniona nikiendelea na safari yangu
No comments:
Post a Comment