
NILIMDANGANYA MKE WANGU NIMEFUKUZWA KAZI KUMBE NNALIKIZO MIEZI 3 SEHEMU YA 06 Lakini kabla hata sijafungua mlango nikamuona mwanangu kajikunyata pembeni ya ukuta, mvua inamnyeshea kajiinamia na begi lake lashule kalikumbatia huku analia, aisee pombe ilikata,, Nilitembea taratibu nikamkumbatia mwanangu machozi yalinitoka ,mwanangu nae alikuwa analia tu ,nikam beba na kuingia nae ndani ,nilim badilisha nguo na nikamvalisha masweta ili apate joto kidogo, na nikatoka na mvua yangu nikaenda kumnunulia chips na maziwa ya moto ili ale maana tokea saa Tisa aliporudi shule hajala kitu mpaka muda huo, Niliporudi nikiwa na chips na maziwa nikamuona mwanangu anatetemeka japo kavaa koti
No comments:
Post a Comment