
???? ????MKE WA MGANGA 16 Tulipoishia “we mwanamke” nilimuita kwa mshangao nikaona amecheka “Nini sasa……vitu nilivyokuambia ulete viko wapi?” aliniuliza nikabaki ninamshangaa huku mdomo wangu ukiwa wazi Endelea Nilimtazama kwa muda mrefu sana nikawa nawaza imekuwaje mpaka ile hali ikanitokea maana haiwezekani hata kidogo, “Wee Zuhura…. Ni nini hiki jamani?” nilimuuliza huku nafsi ikiniambia kwamba yeye ndo yuko sahihi “Kipi?” “Mimi sielewi elewi” nilimuambia, Zuhura alinifuata na kunirushia maji, kimahaba “Kwenda huko, yaani wewe mahaba kidogo tu yashakuchanganya, nenda bhana ukalete hivyo vitu ukirudi tupike nikupe na kimoja, sawa mtoto handsome” alisema akinishika ndevu na kuingia ndani na beseni lake
No comments:
Post a Comment